Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika yakiri kuwepo kwa ubadhirifu wa fedha za wakulima wa tumbaku katika mkoa wa Tabora

Wednesday, May 29, 2013 | comments

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mheshimiwa Adam Malima  ametoa kauli hiyo bungeni  wakati akijibu swali la Mbunge wa Tabora Kaskazini, Mheshimiwa Saffin Sumar  aliyetaka kujua serikali inawasaidiaje wakulima wa zao la tumbaku kutokana na ufisadi mkubwa unaofanywa na chama kilele cha APEX na Chama kikuu cha wakulima wa tumbaku kanda ya magharibi-WETCU kwa kuwaibia wakulima.


Naibu Waziri amesema ubadhrifu na wizi wa fedha kwa wakulima wa tumbaku mkoa wa Tabora ulitokana na viongozi wa WETCU kwa kushirikiana na baadhi ya watendaji wasiokuwa waaminifu wakiwemo watumishi wa mabenki.

Amesema katika kushughulikia tatizo hilo, serikali imeunda kamati maalumu chini ya uenyekiti wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora  ambayo pamoja na mambo mengine itakuwa na jukumu la kuthamini madeni halali ya wakulima.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Designer | Ibrahim Haruna | +255716606570
Copyright © 2011. SAUTI YA VIJIJINI - All Rights Reserved
Template Created by TheDynamite Published by TRJA
Proudly powered by Nativebase Company