Walimu mkoani Tabora wametakiwa kufanya kazi kwa busara, uvumilivu na nidhamu

Saturday, May 18, 2013 | comments




Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Ualimu TABORA, Bwana PETER LABIA amesema kuwa walimu lazima wawe mfano wa kuigwa katika jamii kutokana na kuwa na nidhamu na kufanya kazi yao kwa kutumia busara zaidi.

Bwana LABIA alikuwa akizugumza katika mahafali ya 58 ya Chuo cha Ualimu cha NDALA wilayani NZEGA ambapo aliwatunuku vyeti wahitimu 465 wa mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti.

Akimkaribisha kutunuku vyeti kwa walimu hao watarajiwa, Mkuu wa Chuo cha Ualimu NDALA, Bibi ALFRIDA ABEL amewahimiza wahitimu kuwatii viogozi wa mamlaka watakazoenda kutumikia huku wakidumisha amani, umoja na ushirikiano.

Kwa upande wao, wahitimu wa amfunzo ya ualimu Chuo cha NDALA wameahidi kutoa elimu bora kwa wanafunzi kadri ya uwezo wao kwa kuzingatia mafunzo waliyopata na kwamba watakuwa wapiganaji dhidi ya magonjwa ya UKIMWI na malaria.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Designer | Ibrahim Haruna | +255716606570
Copyright © 2011. SAUTI YA VIJIJINI - All Rights Reserved
Template Created by TheDynamite Published by TRJA
Proudly powered by Nativebase Company