Akiongea katika Bonanza hilo Mwenyekiti wa asasi hiyo BW:ALEX MCHOMVU,alisema,muda umefika kwa waandishi wa Habari wa Tanzania kuungana na kuwatetea Wananchi wa vijijini ambao wao ndio asilimia kubwa ya Taifa letu.Ameongeza kusema kuandika Habari za vijijini ni kama Kujitoleo maana mazingira yake pia ni magumu na Hayamvutii Mwandishi kwenda.
Alimalizia kusema kuwa Wadau Mbalimbali,Serikali na Watu wenye mapenzi mema, wanaombwa kujitokeza kusaidia Asasi hii ya TANZANIA RURAL JOURNALISM kwani ipo kwaajili ya kila mtu kwa lengo la kuleta maendeleo kwa wananchi.
Kulia ni Mkurugenzi wa Radio SAUT FM 96.1 Bw:DOTTO BULENDU EMMANUEL mwenye kofia nyeupe
Bonanza hilo ambalo lilitanguliwa na mashindano mbalimbali kama kufukuza kuku na mpra wa miguu lilimalizika na zawadi kukabidhiwa kwa washindi ambao washindi wa kwanza walipewa sh 20000laki mbili na wa pili laki moja na elfu thelethini 130000.
Vilevile zawadi zilitolewa kwa waashindi wa uandishi bora (TRJA)
Mshindi wa kwanza:Jacob Anthony. Zawadi ni Cheti cha kutambuliwa,Tisheti na Journal ya Africa Communication Research.
Mshindi wa Pili:Abdurahim Msonde.Zawadi ni Tisheti na Journal ya Africa Communication Research.
Mshindi wa Watatu:Denic Mtibulela.Zawadi ni Tisheti na Journal ya Africa Communication Research.
Wote kutoka katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino(SAUT)
Hizi ndizo zawadi walizo pewa washindi hao....

Post a Comment