Jumla ya wanafunzi 7,338 hawakujiunga katika shule mbalimbali za sekondari za kata wilayani Karagwe mkoni Kagera katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2012

Saturday, May 18, 2013 | comments


Mkuu wa Wilaya ya KARAGWE, DARRY RWEGASIRA  amesema wanafunzi hao hawakujiunga na elimu ya sekondari pamoja na kufaulu mtihani wa taifa katika kipindi hicho.

Pia amebainisha kuwa katika mwaka 2010 wanafunzi waliochaguliwa walikuwa 5,150  Kati ya hao 1,177 hawakuripoti shuleni huku  mwaka 2011 wanafunzi 5,107 walichaguliwa na 2,155 hawakuripoti shule.

RWEGASIRA ameongeza kuwa  katika mwaka 2012 kati ya wanafunzi 8,871 waliochagulia, wanafunzi 4,006 hawakuripoti shuleni.

Hata hivyo, amesema shule nyingi za sekondari katika wilaya hiyo hazina miundombinu iliyodumu kutokana na baadhi ya wazazi kutokuwa na mwamko wa kuchangia maendeleo ya shule.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Designer | Ibrahim Haruna | +255716606570
Copyright © 2011. SAUTI YA VIJIJINI - All Rights Reserved
Template Created by TheDynamite Published by TRJA
Proudly powered by Nativebase Company