Mabaraza ya kata katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora yashindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi

Wednesday, May 29, 2013 | comments




Kutokana na kukosa vitendea kazi sanjari na posho ndogo zinazolipwa wakati wa uendeshaji wa kesi mbali mbali Mabaraza ya kata katika Halmashauri ya  Manispaa ya Tabora yameshindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Katibu wa baraza la kata ya Mbugani Bwana Emmanuel Chambo amesema suala la vitendea kazi kwa mabaraza ya kata limekuwa ni changamoto inayokwamisha utendaji wa kazi zao.
Ameongeza  kuwa wamekuwa wakipokea kesi nyingi zinazowahusu wanandoa lakini wanashindwa kuzitolea  maamuzi sahihi kutokana na kukosa ushahidi wa kutosha kwani matukio mengi yanakuwa ni ya siri baina yao ndani ya chumba chao.

Bwana Chambo amefafanua kuwa ili haki ya mtu iweze kupatikana ni vizuri vyema kuwa na ushahidi kwa sababu sheria inahusika zaidi panapokuwa na ushahidi. 

Amewataka wananchi kuhakikisha wanakuwa na ushahidi wa kutosha wanapokwenda kufungua kesi katika baraza lolote la kata ili kutolewa maamuzi yanayojitosheleza kwa mujibu wa sheria.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Designer | Ibrahim Haruna | +255716606570
Copyright © 2011. SAUTI YA VIJIJINI - All Rights Reserved
Template Created by TheDynamite Published by TRJA
Proudly powered by Nativebase Company